Tusiwahukumu Changudoa

Tusiwahukumu Changudoa

4.0
  • AuthorJames B. Kalugira
  • PublisherTanzania Educational Publishers Ltd
  • Year2016

Kwa mujibu wa Kamusi ya Kiswahili Sanifu, Changudoa ni “mwanamke anayezunguka mitaani usiku ili kujiuza kwa wanaume kwa ajili ya kupata fedha.”  Wanawake hawa hawapendi kazi hii ya kuuza miili yao bali ni shida tu zimewalazimisha  kufanya kzi  hii, baada ya kukosa  kazi nyingine.  Katika nchi hii wanaitwa majina mbalimbali kama vile,  Malaya, wahuni, watenda dhambi n.k. Wao wenyewe  wanasikitishwa na jamii kuwaona hivyo na kuwahukumu hivyo. Kwao, hii ni kazi inayowawezesha kuisha na kupata mahitaji yao ya lazima.

 Wanawake hawa  kutokana na kuzidiwa na hali ya maisha wanatamani kupata, lakini, kazi hazipatikani, maana  ili  kupata kazi unatakiwa kujuana na watu, lakini, dada hao hawana watu wa kuwasaidia kupata kazi, hawana pesa za kuhonga kupata kazi. Wanatamani kuolewa ili kuwa na familia zao, kuwa na watoto wao, kuitwa mama fulani au kuitwa yule mama mume wake ni fulani, ndoto zao zinafifia kidogokidogo, matarajio yao ya kuolewa na kutunza familia yanaishia kwenye mateso makali kama ya kuchomwa na mwiba! Matarajio na ndoto zao nzuri zinazimwa.

Katika kitabu hiki, mwandishi ametumia kalamu yake  kujenga hoja ya  kuwatetea  changudoa dhidi ya kuhudumiwa  bila kusikilizwa  na kutoa  mwito  kwa  kila mmoja, kwenye nafasi yake aweze kuwasaidia  ili kutokana na adha hii. Aidha, mwandishi anaamini kuwa,  kila mtu anaweza kubadilisha tabia na mwonekano kwenye jamii endapo  atasikilizwa na kuwezeshwa kama ilivyo kwenye nchi zilizoendelea kama vile, Marekani anakoishi na kufanyakazi mwandishi

Pay with DPO

dpo
Book Title Tusiwahukumu Changudoa
Author James B. Kalugira
ISBN 978-9987-671-60-1
Edition Language
Date Published 2023-12-12
Publisher Tanzania Educational Publishers Ltd
Pages 78
Chapters 12

Related Books

Penzi liliponzwa
Penzi liliponzwa
  • RIWAYA
Tzs5,000.00 Tzs5,000.00
View
Rita Koku
Rita Koku
  • RIWAYA
Tzs5,000.00 Tzs5,000.00
View