Maisha na Ujasiri wa Mjane

Maisha na Ujasiri wa Mjane

4.0
  • AuthorTheophilda Tinkasimire Tikawa
  • PublisherTanzania Educational Publishers Ltd
  • Year2015

Bibi Theophilda Tinkasimire Tikawa, mwandishi wa kitabu
hiki kinachosimulia maisha yake tangu kuzaliwa, kukua,
kusoma shule, kuolewa, kuajiriwa, kufiwa na mume na hatimaye
kufiwa na wazazi wake, ni mama mjane jasiri, mcha Mungu,
mpambanaji, mpenda maendeleo na Mwalimu aliyependa
sana watoto nchini wapate elimu. Ipo mifano hai ya watoto
aliowasaidia na kuwahimiza wasome kwa uwezo wao wote
na sasa ni Maprofesa na Madaktari. Kitabu hiki kinaongelea
safari ya kishujaa ya maisha ya Mwalimu Theophilda ambaye
kwangu binafsi amekuwa mfano wa wanawake wasiokubali
kubweteka na badala yake kujisimamia, kuweka malengo na
mikakati ya maisha na kuisimamia kijasiri licha ya changamoto
mbalimbali hasa za unyanyaswaji wa kijinsia zinazowakabili
akina mama na, hasa, wajane, na waliozaliwa katika mazingira
magumu yaliyojaa mila na desturi za kuwanyanyapaa watoto
wa kike.
Mwalimu Theophilda aliwapenda na kuwaheshimu wazazi
wake wote. Alikuwa na baba wawili: baba mzazi na baba mlezi
aliyempata kwa mujibu wa mila na tamaduni za kabila lake
kama utakavyogundua ukisoma kitabu hiki. Kuolewa kwa
Bi. Theophilda akiwa na umri mdogo na baadaye kufiwa na
mume mapema akiwa na umri mdogo wa miaka 37 lilikuwa
pigo kubwa kwake, lakini, kwa ushupavu wake na msimamo
mkali aliamua kutoolewa tena na kuwalea watoto wake
Bruno, Felix, Letisia na Victor ambao walikuwa bado wadogo.

Pay with DPO

dpo
Book Title Maisha na Ujasiri wa Mjane
Author Theophilda Tinkasimire Tikawa
ISBN 978 9987 426 21 8
Edition Language Kiswahili
Date Published 2015-07-11
Publisher Tanzania Educational Publishers Ltd
Pages 201
Chapters 40

Related Books

Pius Bakengera Ngeze Maisha yake na Baada ya Miaka 70
Pius Bakengera Ngeze Maisha yake na Baada ya Miaka 70
  • BIOGRAPHY AND AUTOBIOGRAPHY
Tzs5,000.00 Tzs5,500.00
View
Maisha Yangu: Alhaji Abubakari R. Galiatano
Maisha Yangu: Alhaji Abubakari R. Galiatano
  • BIOGRAPHY AND AUTOBIOGRAPHY
Tzs5,000.00 Tzs5,500.00
View