KILIMO CHA PAMBA TANZANIA

KILIMO CHA PAMBA TANZANIA

4.0
  • AuthorPius B. Ngeze
  • PublisherTanzania Educational Publishers Ltd
  • Year2010

1. Historia ya pamba nchini
Pamba iliingizwa Tanganyika na Wamisionari na Wafanyabiashara wa
Kijerumani wakati wa utawala wa Wajerumani wa nchi hii katika karne ya
19. Tanganyika ikaanza kupanda pamba (jina sahihi ni mipamba, yaani,
mimea inayozaa pamba) kabla ya mwaka 1900 na ilianza kuuza zao hili
kwenye masoko ya nje mwaka 1920. Uzalishaji wa pamba umeongezeka
haraka tangu 1950.
2. Mazingira ya pamba
Pamba ni zao ambalo hustawi vizuri katika sehemu kubwa ya nchi yetu.
Hustawi katika udongo wa aina mbalimbali mradi tu maji yawe
yanapenya kwa urahisi na usiwe na asidi. Kiasi cha milimita 500 (inchi ishirini)
za mvua hustawisha pamba vema, kama ikinyesha kwa mpangilio
mzuri. Mwinuko wa kuanzia usawa wa bahari hadi mita1,372 (futi
4,500) ndiyo hasa hufaa kwa ustawishaji wa pamba.

Pay with DPO

dpo
Book Title KILIMO CHA PAMBA TANZANIA
Author Pius B. Ngeze
ISBN 978 9987 07 022 0
Edition Language
Date Published 2010-04-20
Publisher Tanzania Educational Publishers Ltd
Pages 94
Chapters 7

Related Books

Banana and their Management
Banana and their Management
  • KILIMO CHA MAZAO (MORDEN CROPS HUSBANDRY)
Tzs5,000.00 Tzs6,000.00
View
COTTON IN TANZANIA: Breaking the Jinx
COTTON IN TANZANIA: Breaking the Jinx
  • KILIMO CHA MAZAO (MORDEN CROPS HUSBANDRY)
Tzs5,000.00 Tzs6,000.00
View