JIFUNZE KUSTAWISHA MTAMA

JIFUNZE KUSTAWISHA MTAMA

4.0
  • AuthorPius B. Ngeze
  • PublisherTanzania Educational Publishers Ltd
  • Year2004

Mtama ni nafaka muhimu sana katika nchi za tropiki na za tropikiusu.

Ni zao linaloweza kustawi hata katika udongo fukara na hustahimili ukame.

Kati ya aina zote za nafaka, mtama ndio hustahimili zaidi ukame. Mtama una matumizi mengi.

Lakini, hasa hutumika kwa chakula cha binadamu na mifugo, kutengeneza aina mbalimbali za vinywaji na kadhalika.
Kutokana na ustahimilivu wake kwa ukame, serikali nyingi sasa hushawishi wakulima walio katika sehemu

zinazopata mvua chache kuacha kulima mahindi na badala yake wapande mtama. Katika sehemu hizo,

mtama hutoa mavuno mengi kuliko mahindi. Mahindi yanahimizwa yapandwe katika sehemu zenye

mvua za kutosha.Vituo vya Utafiti vya Kilimo vimekuwa vikitafiti aina bora za mtama zinazozaa sana,

ambazo ni kinzani au hazishambu-liwi sana na magonjwa na wadudu waharibifu na ambazo

hazipendwi sana na ndege. Utafiti huo bado unaendelea. Kwa hiyo, ni juu ya wakulima kuitaka

serikali yao kuhakikisha kuwa mbegu bora zaidi zinazopatikana nchini kwa kiasi cha kutosha.

Mabwana shamba wana wajibu wa kuwasaidia wakulima katika jambo hili. Ni juu ya wakulima

kumuuliza Bwana au Bibi shamba wao aina ya mtama iliyo bora zaidi na wapi inapatikana.

Pay with DPO

dpo
Book Title JIFUNZE KUSTAWISHA MTAMA
Author Pius B. Ngeze
ISBN 978 9987 671 97 7
Edition Language Kiswahili
Date Published 2003-01-01
Publisher Tanzania Educational Publishers Ltd
Pages 89
Chapters 5

Related Books

Banana and their Management
Banana and their Management
  • KILIMO CHA MAZAO (MORDEN CROPS HUSBANDRY)
Tzs4,000.00 Tzs5,000.00
View
COTTON IN TANZANIA: Breaking the Jinx
COTTON IN TANZANIA: Breaking the Jinx
  • KILIMO CHA MAZAO (MORDEN CROPS HUSBANDRY)
Tzs4,000.00 Tzs5,000.00
View